‘Ni kitu gani cha kwanza ili uweze kuandika?’

Habari za leo.

Karibu waandishigroup, leo nina furaha sana, tangu nimeanza kushughulika na blogu hii nimetimiza mwezi mmoja.

Kama ungeniuliza swali. Ni kitu gani cha kwanza ili uweze kuandika?’

Kabla sijakujibu kuna usemi unasema ‘fanya vitu vya kwanza kwanza’  namaanisha kuwa kati ya vingi ulivyonavyo kuna ambavyo vinachukua nafasi ya kwanza kabla ya vingine. Hivyo katika uandishi kuna vitu ambavyo itabidi uvifanye kwanza kabla ya vingine.

Jibu ni rahisi kuliko unavyoweza kufikiri.  ‘anza kuandika’

Kuanza ndio somo gumu kabisa unaloweza kujifunza. Na ni rahisi kusema kuliko unavyoweza kulifanya.

Tatizo ni kwamba ubongo huwa unafanya kazi nzuri ya kukuletea sababu/ visingizio usifanye kitu fulani ambacho kinakupa changamoto na jinsi unavyozidi kusubiri ndio jinsi unajenga sababu nyingi za kutofanya jambo hilo.

Tangu mwezi uliopita nimefanyia kazi blogu hii ili kuwasaidia wale wanaoanza kuandika katika hatua zao za kujenga uwezo wao. Hakuna tena cha kukuzuia na milango ipo wazi kabisa.

Haijalishi kama una mawazo mengi na hujui wazo lipi ni bora kabisa, au hata kama huna wazo kabisa. Waandishigroup itakufanya ugundue ni upande upi uwe na kundi gani la hadhira.

Karibu tuendelee kuwa pamoja. Anza kuandika na anza leo. Nakupa wazo, andika unataka kuandika kuhusu nini na lengo lako ni nini. Umeona picha hapo juu, kuna watu wameamua kukimbia huku wamevaa suti. wengine wamevaa tai, wengine viatu vya moka. Huhitaji kuwa na kila kitu ili kuanza. Cha muhimu ni kuanza tuu.

Leave a comment